Leviticus 27:1-6
Kukomboa Kile Kilicho Cha Bwana
1 Bwana akamwambia Musa, 2 a“Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Kama mtu yeyote ataweka nadhiri maalum ili kuweka watu wakfu kwa Bwana, kwa kutoa kiasi cha thamani inayolingana, 3 bthamani ya kukomboa mwanaume mwenye kati ya umri wa miaka ishirini na miaka sitini itakuwa shekeli hamsini ▼▼ Shekeli 50 za fedha ni sawa na gramu 600.
za fedha, kulingana na shekeli ya mahali patakatifu; 4ikiwa ni mwanamke, weka thamani yake kwa shekeli thelathini. ▼▼ Shekeli 30 za fedha ni sawa na gramu 360.
5 eKama ni mtu mwenye umri wa miaka kati ya mitano na ishirini, weka thamani ya mwanaume kuwa shekeli ishirini, ▼▼ Shekeli 20 za fedha ni sawa na gramu 240.
na mwanamke shekeli kumi. ▼▼ Shekeli 10 za fedha ni sawa na gramu 120.
6 hKama ni mtu mwenye umri kati ya mwezi mmoja na miaka mitano, weka thamani ya mwanaume kuwa shekeli tano za fedha, na ile ya mwanamke kuwa shekeli tatu ▼▼ Shekeli tatu za fedha ni sawa na gramu 36.
za fedha.
Copyright information for
SwhKC